Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Nzega leo limepitisha Mpango na Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2026/2027 yenye jumla ya Shilingi bilioni 50.9 kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli mbalimbali za maendeleo na utoaji wa huduma kwa wananchi.
Bajeti hiyo inatarajiwa kugharamia mishahara ya watumishi, matumizi ya kawaida pamoja na miradi ya maendeleo katika sekta mbalimbali ikiwemo Elimu, Afya, Viwanda na Biashara pamoja na Utawala.
Kati ya fedha hizo, Shilingi bilioni 32.19 ni kwa ajili ya Mishahara (PE), Shilingi bilioni 1.89 kwa Matumizi ya Kawaida (OC), huku Shilingi bilioni 11.98 zikitengwa kwa Miradi ya Maendeleo kupitia ruzuku ya Serikali Kuu na Wahisani.
Aidha, Halmashauri imekadiria kukusanya Shilingi bilioni 4.87 kutoka katika vyanzo vya mapato ya ndani (own source), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuimarisha ukusanyaji wa mapato na kuongeza uwezo wa kifedha wa Halmashauri.
Kupitishwa kwa mpango na bajeti hiyo kunaonesha dhamira ya Halmashauri ya Wilaya ya Nzega kuendelea kusimamia maendeleo ya wananchi kwa kuzingatia uwazi, uwajibikaji na matumizi sahihi ya rasilimali za umma.








Halmashauri ya Wilaya ya Nzega (Kata ya Utwigu kijiji cha Mwambaha Lubisu )
Anuani ya Posta: S.L.P 4
Telephone: 026 2692349
Simu ya Kiganjani: 0765600994
Barua pepe: md@nzegadc.go.tz
Hati miliki Halmashauri ya Wilaya ya Nzega @ 2017. Haki zote zimehifadhiwa