• Malalamiko |
    • Wasiliana na sisi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe kwa Watumishi |
Nzega District Council
Nzega District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nzega

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
    • Vitengo
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • sheria
      • Nyuki
      • TEHAMA
  • Fulsa za Uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
    • Vivutio katika Kilimo
    • Vivutio vya Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Utamaduni na Michezo
    • Maji
    • Kilimo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha Mipango na Utawala
      • kamati ya uchumi kazi na mazingira
      • kamati ya Elimu afya na maji
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Madili
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • kuonana na mwenyekiti wa halmashauri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video za shughuli za ofisi
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

NAWAAGIZENI HALMASHAURI ZOTE NCHINI HAKIKISHENI “MATERIALS” YOTE YANANUNULIWA TOKA VIWANDA VYA NDANI

Posted on: October 23rd, 2018


Mhe. Seleman Jafo Waziri Ofisi ya Rais Tawala  za Mikoa na Serikali za Mitaa aagiza halmashauri zote na taasisi zote nchini kutumia viwanda vya ndani kununua vifaa muhimu vya ujenzi kama , Mabati,Nondo Saruji na Vigae vya ndani. Aliyasema hayo alipotembelea mradi wa ujenzi wa jengo la uzazi la kinamama  katika Hospitali ya Wilaya ya Nzega leo tarehe 23/10/2018 .

‘’Wakati mwingine mtu ukimwamini sana mwisho wa siku watu wanaharibu ndilo tatizo letu’’ aliyasema hayo alipokuwa katika kuongea na kamati ya ujenzi wa Hospital ya wilaya ya Nzega.  Mhe. Selemani Jafo aliwataka wakurugenzi wa Halmashauri zote mbili kuhakikisha kuwa ujenzi  huo unakuwa na thamani ya Pesa, akisema kuwa ni vema pesa yote itakayobaki mara baada ya ujenzi wa wadi ya  mama na watoto ya kisasa ioneshe “value for money” katika kila jingo litakalokarabatiwa. Pesa hiyo hapo awali ilikuwa itumike kwa maandalizi ya  ujenzi wa hospital ya Wilaya katika maeneo ya karitu.

Aidha mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Nzega  ndugu Sekiete S Yahaya alimweleza Waziri kuwa watahakikisha wanasimamia ujenzi huo kwa umakini na kuwa fedha itakayobaki mara baada ya kujenga wadi ya uzazi itakarabati wadi kubwa ya Bima ya Afya, wadi ya wazazi, X-Ray na wadi ya Watoto.

Mhe. Seleman Jafo alisifia shughuli zote zinazofanyika katika Halmashauri za wilaya ya Nzega(Mji na Wilaya), lakini aliwataadharisha kuwa wasibweteke kwa kazi hizo zilizoonekana Busondo,Unambewa, Lusu,Mwangoye na Zogolo.  Tunataka tujenge kitu kizuri zaidi na nitakapokuja hapa tena nikute kitu cha tofauti,’ Mhe. Waziri alisema. Lakini pia aliridhishwa na aina ya tofali zinazotumika katika ujenzi wa majengo hayo kwani inaonekana sehemu nyingine tofali zimekuwa zikileta nyufa mara baada ya Ujenzi kukamilika .

Pia Mhe. Waziri alifurahishwa na kitendo cha ununuzi wa vifaa kutoka katika viwanda vya ndani. Alielekeza kuwa ununuzi wote wa Sementi, Mabati na Nondo ufanywe toka viwanda vyetu vya ndani kwani kuna viwanda vingine kama kilichopo Mkuranga na Kibaha Magodauni yamejaa nondo lakini wengine bado wananunua Nondo toka nje ya nchi. Fedha bilioni 33 zimesahaanza kutolewa kwa ajili ya ujenzi wa Halmashauri hivyo basi alizitaka halmashauri zote nchini kununua bidhaa hiyo kwenye viwanda hivyo. Wizara yake inasimamia miundombinu mingi hivyo hatakubali kuona viwanda vya ndani vinakufa.

Aliwataka wakurugenzi kuongeza mwendo katika ujenzi na ukarabati kwani bado wako nyuma sana. Mhe.Waziri aliwashukuru kwa kumsikiliza na kasha alichukua picha za pamoja na watumishi na kasha aliendelea na safari yake kuelekea Dodoma.

Matangazo

  • MATOKEO YA PSLE 2020/DARASA LA SABA December 18, 2020
  • FOMU ZA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA SHULE ZA SEKONDARI NZEGA DC December 18, 2020
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021 TOKA NZEGA DC WAVULANA NA WASICHANA December 18, 2020
  • FOMU YA MAOMBI YA UUZAJI WA VIWANJA HALMASHAURI YA WILAYA YA NZEGA KATIKA MAENEO YA NATA, ITOBO, BUKENE NA NDALA July 12, 2019
  • Angalia yote

Habari mpya

  • MITI ZAIDI YA ELFU MOJA YAPANDWA

    January 05, 2020
  • MHE. AGGREY MWANRI ALIAGIZA JESHI LA POLISI KUMKAMATA AFISA AMCOS NZEGA DC

    December 23, 2019
  • Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Nzega Akabidhi Mikopo yenye Thamani ya Shilingi 84,000,000

    February 18, 2019
  • karibuni kuwekeza Nzega DC katika Ranchi, Wanyama na Mazao

    November 23, 2018
  • Angalia yote

Video

HALMASHAURI YA WILAYA YA NZEGA YAHAMISHIA SHUGHULI ZA KIOFISI NDALA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Matukio
  • Habari Mpya
  • Matangazo
  • Zabuni

Kurasa Zinazofanana

  • TAMISEMI
  • KARIBUNI NZEGA YETU
  • twitter
  • Instagram
  • Mkoa wa Tabora
  • Utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana na sisi

    Halmashauri ya Wilaya ya Nzega (Mtaa wa Umbi)

    Anuani ya Posta: S.L.P 4

    Telephone: 026 2692349

    Simu ya Kiganjani: 0784364828

    Barua pepe: md@nzegadc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hati miliki Halmashauri ya Wilaya ya Nzega @ 2017. Haki zote zimehifadhiwa