• Malalamiko |
    • Wasiliana na sisi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe kwa Watumishi |
Nzega District Council
Nzega District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nzega

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
    • Vitengo
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • sheria
      • Nyuki
      • TEHAMA
  • Fulsa za Uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
    • Vivutio katika Kilimo
    • Vivutio vya Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Utamaduni na Michezo
    • Maji
    • Kilimo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha Mipango na Utawala
      • kamati ya uchumi kazi na mazingira
      • kamati ya Elimu afya na maji
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Madili
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • kuonana na mwenyekiti wa halmashauri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video za shughuli za ofisi
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
      • Elimu Msingi Kovid 19
        • Boma
        • kupaua
        • uwekaji wa rangi
      • Sekondari Picha Kovid 19
        • Boma
        • kupaua
        • Kuweka Rangi
      • Afya Picha Kovid 19
        • Boma
        • kupaua
        • uwekaji wa rangi

WAHESHIMIWA MADIWANI NZEGA WAHITIMISHA MAFUNZO YA UONGOZI KWA KUSISITIZWA TEHAMA NA MAADILI

Posted on: January 21st, 2026

Mafunzo ya kuwajengea uwezo Madiwani wa Halmashauri ya Mji wa Nzega na Halmashauri ya Wilaya ya Nzega yamehitimishwa leo kwa msisitizo mkubwa juu ya matumizi sahihi ya Teknolojia  (TEHAMA) pamoja na kuzingatia maadili katika uongozi na utumishi wa umma.

Katika siku ya tatu na ya mwisho ya mafunzo hayo, Madiwani wameelekezwa kutumia TEHAMA kama nyenzo ya kuongeza uwazi, ufanisi na kasi ya utoaji wa huduma kwa wananchi, huku wakikumbushwa kuwa matumizi ya teknolojia bila kuzingatia maadili yanaweza kuathiri maendeleo yanayokusudiwa.

Mafunzo hayo pia yameweka msisitizo kwa Madiwani kutambua mipaka ya majukumu yao, kwa kuelekezwa kutokuingilia kazi za kitaalamu zinazotekelezwa na wataalamu wa Halmashauri, ili kulinda weledi, uwajibikaji na ubora wa maamuzi katika utekelezaji wa majukumu ya umma.

Akiwasilisha mada ya maadili, mkufunzi kutoka Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma ameeleza umuhimu wa viongozi wa umma kujiepusha na migongano ya maslahi, akifafanua kuwa kiongozi hapaswi kushiriki katika maamuzi au michakato inayohusisha maslahi yake binafsi au ya watu wa karibu, kwani hali hiyo huathiri utekelezaji wa wajibu wake kwa manufaa ya umma.

Aidha, ilielezwa kuwa Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma inawataka viongozi kuzingatia uadilifu na kujiepusha na mahusiano ya kibiashara yanayoweza kuathiri uwajibikaji wao. Kwa mujibu wa sheria hiyo, kiongozi wa umma hapaswi kuingia au kushiriki katika biashara au mikataba na Halmashauri anayoihudumia au yenye mamlaka juu yake, ili kuepuka mgongano wa maslahi na kulinda maslahi ya umma.

Mafunzo hayo ya siku tatu yamehitimishwa kwa wito kwa Madiwani kutumia maarifa na ujuzi walioupata kuimarisha uongozi, kuzingatia maadili, na kutumia TEHAMA kwa njia itakayochochea maendeleo endelevu na ustawi wa wananchi wa Nzega.


Matangazo

  • MATOKEO YA PSLE 2025/DARASA LA SABA-MKOA WA TABORA November 05, 2025
  • ORODHA YA MAJINA WALIOITWA KWENYE USAILI JIMBO LA BUKENE NA NZEGA VIJIJINI October 11, 2025
  • TANGAZO-WAMILIKI WA MAGARI September 30, 2025
  • ORODHA YA MAJINA YA MAKARANI WALIOITWA KWENYE USAILI JIMBO LA NZEGA VIJIJINI July 18, 2022
  • Angalia yote

Habari mpya

  • WAHESHIMIWA MADIWANI NZEGA WAHITIMISHA MAFUNZO YA UONGOZI KWA KUSISITIZWA TEHAMA NA MAADILI

    January 21, 2026
  • MADIWANI NZEGA WAPATA ELIMU YA MIRADI SHIRIKISHI, MIPANGO NA BAJETI

    January 20, 2026
  • MADIWANI NZEGA WAHIMIZWA KUTUMIA MAFUNZO KUBUNI VYANZO VIPYA VYA MAPATO

    January 19, 2026
  • MDAHALO:IPI NAFASI YA VIJANA KATIKA KUZIFIKIA FURSA ZINAZOMZUNGUKA

    January 12, 2026
  • Angalia yote

Video

UJENZI WA MIUNDOMBINU YA ELIMU HALMASHAURI YA WILAYA YA NZEGA YAENDELEA KWA KASI
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Matukio
  • Habari Mpya
  • Matangazo
  • Zabuni

Kurasa Zinazofanana

  • TAMISEMI
  • KARIBUNI NZEGA YETU
  • twitter
  • Instagram
  • Mkoa wa Tabora
  • Utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana na sisi

    Halmashauri ya Wilaya ya Nzega (Kata ya Utwigu kijiji cha Mwambaha Lubisu )

    Anuani ya Posta: S.L.P 4

    Telephone: 026 2692349

    Simu ya Kiganjani: 0765600994

    Barua pepe: md@nzegadc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hati miliki Halmashauri ya Wilaya ya Nzega @ 2017. Haki zote zimehifadhiwa