• Malalamiko |
    • Wasiliana na sisi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe kwa Watumishi |
Nzega District Council
Nzega District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nzega

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
    • Vitengo
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • sheria
      • Nyuki
      • TEHAMA
  • Fulsa za Uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
    • Vivutio katika Kilimo
    • Vivutio vya Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Utamaduni na Michezo
    • Maji
    • Kilimo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha Mipango na Utawala
      • kamati ya uchumi kazi na mazingira
      • kamati ya Elimu afya na maji
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Madili
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • kuonana na mwenyekiti wa halmashauri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video za shughuli za ofisi
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
      • Elimu Msingi Kovid 19
        • Boma
        • kupaua
        • uwekaji wa rangi
      • Sekondari Picha Kovid 19
        • Boma
        • kupaua
        • Kuweka Rangi
      • Afya Picha Kovid 19
        • Boma
        • kupaua
        • uwekaji wa rangi

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Nzega Akabidhi Mikopo yenye Thamani ya Shilingi 84,000,000

Posted on: February 18th, 2019


Mwenyekikiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Nzega Mhe. Kiwele Michael Bundala amekabidhi mikopo kwa vikundi 52 ikiwa wanawake vikundi 32 na vijana vikundi 20. Zoezi hilo limefanyika leo katika ukumbi mdogo wa Halmashauri ya Wilaya ya Nzega kwa Kukabidhi Shilingi Milioni themanini nan ne.

Akisoma risala kwa Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya Kaimu Afisa Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Wilaya Ndugu Robert Mwanga alisema kuwa katika mwaka wa fedha 2018/19 Halmashauri ina mpango wa kutoa mikopo kufikia kiasi cha shilingi 225,140,000/= ikiwa vijana ni Shilingi 88,040,000/=, wanawake 88,040,000/= na walemavu ni shilingi 49,000,000/=.  Alisema kuwa fedha hii inatoka katika mapato ya ndani kwa mwaka huu wa fedha sawa na asilimia 10 ya mapato yote.

Aidha afisa huyo alionesha mafanikio kuwa ni pamoja na kutoa kiasi cha shilingi milioni 132,500,000/= mpaka kufikia robo hii ya tatu ambayo ni sawa na asilimia 59% ya lengo la mwaka huu wa fedha. Leo hii vikundi vikundi 20 vya vijana vimepata kiasi cha shilingi  42,000,000/= na vikundi vya kinamama kiasi cha shilingi 42,000,000/= kufanya jumla ya shilingi 84,000,000/=.

Halmashauri imefanikiwa kutoa elimu ya kutosha kwa wananchi juu ya elimu ya ujasilamali,uibuaji miradi pamoja na uendelezaji wake. Mpaka kufikia robo ya tatu vikundi 89 vimenufaika na mikopo hiyo sawa na ongezeko la asilimia 83% ukilinganisha na mwaka wa fedha uliopita.

Akielezea matatizo yanayojitokeza katika zoezi hilo ni pamoja na vikundi vya walemavu kutojitokeza kuomba mikopo,ucheleweshaji wa marejesho kwa baadhi ya vikundi,uhaba wa rasilimali fedha  na maombi ya mikopo kuwa makubwa  kuliko fedha iliyopo. Mahitaji ya vikundi ni kiasi cha shilingi = 206,000,000/= uwezo wa halmashauri ni kiasi cha shilingi 184,000,000/- sawa na silimia 41% ya maombi  yote.

Akihitimisha risala hiyo Kaimu Maendeleo ya jamii Wilaya ndugu Robert Mwanga alimuomba mwenyekiti kutumia nafasi yake kuwashawishi waheshimiwa madiwani kuwahamasisha wananchi kuwa na moyo wa kurejesha kwa wakati ili kutoa nafasi kwa wananchi wengine kuweza kukopa.

Aidha Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya Mhe. Kiwele Michael Bundala aliwasisitiza wanavikundi kuwa na matumizi mazuri ya fedha, “serikali imetoa fedha hii ili kuwafanya wananchi wake kuufikia uchumi wa kati’’ hivyo aliwataka waitumie fedha hiyo kwa faida kubwa, wala hawakupewa fedha hiyo kwa maana ya kununua chakula nyumbani,kwenda baa, kusuka nywele na kununua vitenge. Aliwaomba wasimamie malengo yote waliyojiwekea ili kuleta tija.

Akiendelea kuongea Mheshimiwa Kiwele alisema kuwa walemavu si wengi kutoka maeneo ya kata moja  hivyo tutaandaa utaratibu wa kuwapata ili watumie fursa hii katika kuzalisha kuliko kukaa bure. Pamoja na hayo Mhe. Alisisitiza kuwa vikundi vingi vimekuwa na maandiko yanayofanana hivyo aliwaomba  wawe na ubunifu katika kuandaa maandiko.

Akisema na wananchi hao aliwataka wanavikundi wote watakaofanya marejesho vizuri ndani ya miezi 6 watapewa kipaumbele katika  kupewa mikopo mingine.

Kwa upande wa wanavikundi wao waliishukuru serikali kwa namna inavyowajali wananchi wanyonge.

Mkurugenzi mtendaji(W) ndugu Sekiete S Yahaya aliwaasa wanavikundi kutotumia vibaya fedha hizo, tumieni taratibu mlizojiweka katika kutumia fedha hizo,’ alisema mkurugenzi. Katika kuhitimisha kikao hicho Mkurugenzi alisema kuwa katika kutekeleza ilani ya chama cha mapinduzi mikopo hii si kama sadaka msikitini ama kanisani hii ni fedha unayopewa ili uirejeshe na ndiyo maana fedha hii haina riba kwa asilimia miamoja.aliwataka wananchi kutumia vizuri mikopo hii ili kuondoa umasikini na kuwa na uwezo wa kujitegemea. Aliahidi kuwa pamoja na kupewa mikopo hii kama taasisi haitaishia hapo bali ni pamoja na kuwatembelea huko walipo. Aliwatakia utendaji mwema katika shughuli zao.

Matangazo

  • MATOKEO YA PSLE 2020/DARASA LA SABA December 18, 2020
  • MAJINA YA MAKARANI WALIOITWA KWENYE USAILI JIMBO LA NZEGA VIJIJINI December 18, 2020
  • MATOKEO YA USAILI WA WATENDAJI DARAJA LA III July 08, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA WATENDAJI DARAJA LA III July 08, 2022
  • Angalia yote

Habari mpya

  • ZIARA YA MAKAMU WA RAIS WA JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA HALMASHAURI YA WILAYA YA NZEGA

    October 08, 2024
  • KAMATI YA FEDHA UTAWALA NA MIPANGO YAMPONGEZA MKURUGENZI KWA USIMAMIZI WA MIRADI

    September 05, 2024
  • UBORESHAJI WA LISHE UWE NA MATOKEO CHANYA YA KIELEIMU

    February 07, 2024
  • UBORESHAJI WA LISHE UWE NA MATOKEO CHANYA YA KIELEIMU

    February 07, 2024
  • Angalia yote

Video

HALMASHAURI YA WILAYA YA NZEGA YAHAMISHIA SHUGHULI ZA KIOFISI NDALA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Matukio
  • Habari Mpya
  • Matangazo
  • Zabuni

Kurasa Zinazofanana

  • TAMISEMI
  • KARIBUNI NZEGA YETU
  • twitter
  • Instagram
  • Mkoa wa Tabora
  • Utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana na sisi

    Halmashauri ya Wilaya ya Nzega (Kata ya Utwigu kijiji cha Mwambaha Lubisu )

    Anuani ya Posta: S.L.P 4

    Telephone: 026 2692349

    Simu ya Kiganjani: 0765600994

    Barua pepe: md@nzegadc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hati miliki Halmashauri ya Wilaya ya Nzega @ 2017. Haki zote zimehifadhiwa