• Malalamiko |
    • Wasiliana na sisi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe kwa Watumishi |
Nzega District Council
Nzega District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nzega

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
    • Vitengo
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • sheria
      • Nyuki
      • TEHAMA
  • Fulsa za Uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
    • Vivutio katika Kilimo
    • Vivutio vya Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Utamaduni na Michezo
    • Maji
    • Kilimo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha Mipango na Utawala
      • kamati ya uchumi kazi na mazingira
      • kamati ya Elimu afya na maji
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Madili
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • kuonana na mwenyekiti wa halmashauri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video za shughuli za ofisi
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
      • Elimu Msingi Kovid 19
        • Boma
        • kupaua
        • uwekaji wa rangi
      • Sekondari Picha Kovid 19
        • Boma
        • kupaua
        • Kuweka Rangi
      • Afya Picha Kovid 19
        • Boma
        • kupaua
        • uwekaji wa rangi

MKUU WA WILAYA YA NZEGA AADHIMISHA SIKU YA KUZALIWA RAIS SAMIA KWA VITENDO: ATEMBELEA SHULE, ATOA ZAWADI, ATOA ONYO KALI KWA WANAOKIUKA HAKI YA ELIMU NA KUONGOZA KAMPENI YA UPANDAJI MITI

Posted on: January 27th, 2026

Leo tarehe 27 Januari, ikiwa ni siku ya kuzaliwa ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Mkuu wa Wilaya ya Nzega, Mheshimiwa Naitapwaki L. Tukai, ameazimisha siku hii muhimu kwa vitendo vya kijamii vinavyoakisi utu, uzalendo wa kweli na uongozi wa mfano.

Katika kuenzi maono na mchango mkubwa wa Rais Samia katika kuimarisha sekta ya elimu na utunzaji wa mazingira, Mheshimiwa Tukai alitembelea Shule ya Sekondari Ikindwa, iliyopo Kata ya Ikindwa, Halmashauri ya Wilaya ya Nzega. Ziara hiyo ililenga kuhamasisha wanafunzi, walimu na jamii kwa ujumla kuhusu umuhimu wa elimu, malezi bora na kulinda mazingira.

Katika tukio hilo, Mkuu wa Wilaya alishirikiana na Ofisi ya Mbunge wa Bukene, ambapo Mheshimiwa Mbunge John Luhende aliwakilishwa na Katibu wake, Bw. Abubakary Bukuku. Kupitia ushirikiano huo, waliweza kukabidhi zawadi mbalimbali za kielimu kwa wanafunzi wa Kidato cha Kwanza, zikiwemo madaftari, kalamu, mpira kwaajili ya wavulana na wasichana,mabegi ya shule, rula pamoja na sare za shule. Zawadi hizo zilitolewa kama sehemu ya kuwahamasisha wanafunzi kuendelea na masomo pamoja na kupunguza mzigo kwa wazazi na walezi.

Mheshimiwa Tukai alitumia fursa hiyo kutoa onyo kali kwa wazazi na walezi wanaowazuia watoto kwenda shule, akisisitiza kuwa kitendo cha kuwanyima watoto haki ya elimu ni kosa la kisheria. Alieleza wazi kuwa hatua kali za kisheria zitachukuliwa mara moja dhidi ya yeyote atakayebainika kuwakatisha watoto masomo, kuwaozesha mapema, kuwapeleka kufanya kazi za mashambani, kuchunga mifugo au kuwatumikisha katika kazi za ndani.

Aidha, aliwahimiza wanafunzi kutoa taarifa pindi wanapobaini kuwepo kwa mwanafunzi aliyepaswa kujiunga na Kidato cha Kwanza lakini amezuiwa na mzazi au mlezi wake. Alisisitiza kuwa Serikali ya Wilaya haitasita kuchukua hatua kali kwa mzazi au mlezi yeyote atakayekiuka haki za mtoto.

Katika kuendeleza ajenda ya taifa ya utunzaji wa mazingira, Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya, kwa kushirikiana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya, Katibu Tawala wa Wilaya pamoja na maafisa kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Nzega, walishiriki zoezi la upandaji wa miti ya kivuli na matunda katika eneo la shule hiyo. Alitoa wito kwa walimu na wanafunzi kuitunza miti hiyo kama sehemu ya kulinda mazingira na kuhakikisha maendeleo endelevu kwa kizazi cha sasa na kijacho.

Baada ya kukamilisha shughuli za kijamii shuleni, Mheshimiwa Tukai alirejea ofisini ambako alikata keki maalum kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Keki hiyo ilitolewa na wafanyabiashara wa Wilaya ya Nzega kama ishara ya kutambua mchango mkubwa wa Rais Samia katika kuwawezesha wafanyabiashara na kuimarisha mazingira bora ya biashara nchini, sambamba na kumtakia maisha marefu, afya njema na mafanikio endelevu katika kulitumikia Taifa.

Maadhimisho haya yamebeba ujumbe mzito unaoonesha kuwa uzalendo wa kweli unaanza kwa vitendo, kwa kulinda haki za watoto, kuwekeza katika elimu na kutunza mazingira yetu.

Mti wa leo ni maisha ya kesho, ni mvua ya kesho, ni maji ya kesho, na ni ardhi salama ya kesho. Anza sasa, mhimize na mwingine.

“Uzalendo ni Kutunza Mazingira, Shiriki Kupanda Miti”

#MazingiraNiUtu


MATUKIO KATIKA PICHA

Matangazo

  • MATOKEO YA PSLE 2025/DARASA LA SABA-MKOA WA TABORA November 05, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA WAKUSANYA MAPATO (REVENUE COLLECTORS) January 26, 2026
  • ORODHA YA MAJINA WALIOITWA KWENYE USAILI JIMBO LA BUKENE NA NZEGA VIJIJINI October 11, 2025
  • TANGAZO-WAMILIKI WA MAGARI September 30, 2025
  • Angalia yote

Habari mpya

  • MKUU WA WILAYA YA NZEGA AADHIMISHA SIKU YA KUZALIWA RAIS SAMIA KWA VITENDO: ATEMBELEA SHULE, ATOA ZAWADI, ATOA ONYO KALI KWA WANAOKIUKA HAKI YA ELIMU NA KUONGOZA KAMPENI YA UPANDAJI MITI

    January 27, 2026
  • WAHESHIMIWA MADIWANI NZEGA WAHITIMISHA MAFUNZO YA UONGOZI KWA KUSISITIZWA TEHAMA NA MAADILI

    January 21, 2026
  • MADIWANI NZEGA WAPATA ELIMU YA MIRADI SHIRIKISHI, MIPANGO NA BAJETI

    January 20, 2026
  • MADIWANI NZEGA WAHIMIZWA KUTUMIA MAFUNZO KUBUNI VYANZO VIPYA VYA MAPATO

    January 19, 2026
  • Angalia yote

Video

UJENZI WA MIUNDOMBINU YA ELIMU HALMASHAURI YA WILAYA YA NZEGA YAENDELEA KWA KASI
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Matukio
  • Habari Mpya
  • Matangazo
  • Zabuni

Kurasa Zinazofanana

  • TAMISEMI
  • KARIBUNI NZEGA YETU
  • twitter
  • Instagram
  • Mkoa wa Tabora
  • Utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana na sisi

    Halmashauri ya Wilaya ya Nzega (Kata ya Utwigu kijiji cha Mwambaha Lubisu )

    Anuani ya Posta: S.L.P 4

    Telephone: 026 2692349

    Simu ya Kiganjani: 0765600994

    Barua pepe: md@nzegadc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hati miliki Halmashauri ya Wilaya ya Nzega @ 2017. Haki zote zimehifadhiwa