• Malalamiko |
    • Wasiliana na sisi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe kwa Watumishi |
Nzega District Council
Nzega District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nzega

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
    • Vitengo
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • sheria
      • Nyuki
      • TEHAMA
  • Fulsa za Uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
    • Vivutio katika Kilimo
    • Vivutio vya Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Utamaduni na Michezo
    • Maji
    • Kilimo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha Mipango na Utawala
      • kamati ya uchumi kazi na mazingira
      • kamati ya Elimu afya na maji
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Madili
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • kuonana na mwenyekiti wa halmashauri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video za shughuli za ofisi
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
      • Elimu Msingi Kovid 19
        • Boma
        • kupaua
        • uwekaji wa rangi
      • Sekondari Picha Kovid 19
        • Boma
        • kupaua
        • Kuweka Rangi
      • Afya Picha Kovid 19
        • Boma
        • kupaua
        • uwekaji wa rangi

UKOSEFU WA GARI ZA KUBEBEA KOKOTO WAPELEKEA HATA LORI ZA MIZIGO KUENDELEZA KAZI

Posted on: November 29th, 2021

"Piga ua garagaza lazima kazi iendelee na hakuna kusimama" ameyasema hayo mkurugenzi wa halmashauri ya Wilaya ya Nzega Wakili Kiomoni Kiburwa Kibamba alipokuwa kwenye ukaguzi wa miradi ya ujenzi wa shule za Sekondari leo.

Mpaka kufikia saa moja jioni msafara wa wataalau wa halmashauri ukijumuisha wakuu wa Idara ulikuwa unaendelea kufanya ukaguzi huo kwa maeneo yote ya shule za sekondari.

Aidha Mkurugenzi Mtendaji, Kiomoni K Kibamba amewataka wakuu wa shule zote kuhakikisha wanaweka taa usiku ili kazi iendelee usiku kucha hii yote imesababishwa na tabia ya wazabuni kuchukua tenda na kutoifanya kwa wakati,hivyo kumlazimu Mkurugenzi Mtendaji kutoa maelekezo kwa wakuu wa shule,watendaji na viongozi wa kijiji kuhakikisha wanatoa ushirikiano wa kutosha vyovyote iwayo ili kuhakikisha siku ya leo majengo yote ambayo hayakuwa yametandika jamvi kama,Mizibaziba,Nkiniziwa,Tongi,Budushi na Magengati yanafanya hivo.

Isitoshe watendaji wakishirikiana na jeshi la jadi la sungusungu wahakikishe wanatumika kubeba tofali na kuleta kokoto katika eneo la ujenzi ili kuepuka ulaghai wa wazabuni wanaoufanya kwa kuchelewesha kazi.

"Hakuna siku iitwayo kesho, kama kuna yeyote aliyewahi kukutana nayo aseme" aliyasema hayo alipokuwa shule ya sekondari Budushi baada ya kuonekana zoezi la ujenzi linasuasua, hiyo ikisababishwa na mzabuni aliyekuwa amechukua tenda kutoleta kokoto na mawe kwa wakati, hivyo kulazimika kuchukua hatua za kutafuta mzabuni mwingine ili kazi iendelee.

Katika ukaguzi huoMkurugenzi mtendaji alimtaka mkuu wa shule ya Magengati na mtendaji wa kijiji  kuhakikisha wanaondoa tofauti zao na kujenga umoja ili kazi hiyo ikamilike kwa wakati. Aidha Mwenyekiti wa kijiji hicho Bi.Halima Salumu Mseluka aliomba msamaha kwa ajili ya viongozi hao walioonekana kutofautiana na kurushiana mpira, baada ya kuonekana kuwa hapakuwa na uwazi juu ya taarifa za ujenzi tofauti na Mwalimu mkuu shule ya sekondari Milamboitobo ambaye alibandika taarifa za matumizi ya fedha ubaoni kwamba kila mmoja anaweza kuona na kusoma.

Shule za Kampala madarasa 3, iPuge madarasa3 na Mwanhala madarasa 3 yalikuwa yamefikia hatua ya kuweka lenta.

Timu ya wakuu wa idara(CMT) imeendelea na zoezi la ukaguzi wa miradi usiku huu katika maeneo ya Karitu,Nata na Sigili.

Imeandaliwa na Isidori Mayagilo

ICTO



Matangazo

  • MATOKEO YA PSLE 2020/DARASA LA SABA December 18, 2020
  • MAJINA YA MAKARANI WALIOITWA KWENYE USAILI JIMBO LA NZEGA VIJIJINI December 18, 2020
  • MATOKEO YA USAILI WA WATENDAJI DARAJA LA III July 08, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA WATENDAJI DARAJA LA III July 08, 2022
  • Angalia yote

Habari mpya

  • ZIARA YA MAKAMU WA RAIS WA JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA HALMASHAURI YA WILAYA YA NZEGA

    October 08, 2024
  • KAMATI YA FEDHA UTAWALA NA MIPANGO YAMPONGEZA MKURUGENZI KWA USIMAMIZI WA MIRADI

    September 05, 2024
  • UBORESHAJI WA LISHE UWE NA MATOKEO CHANYA YA KIELEIMU

    February 07, 2024
  • UBORESHAJI WA LISHE UWE NA MATOKEO CHANYA YA KIELEIMU

    February 07, 2024
  • Angalia yote

Video

HALMASHAURI YA WILAYA YA NZEGA YAHAMISHIA SHUGHULI ZA KIOFISI NDALA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Matukio
  • Habari Mpya
  • Matangazo
  • Zabuni

Kurasa Zinazofanana

  • TAMISEMI
  • KARIBUNI NZEGA YETU
  • twitter
  • Instagram
  • Mkoa wa Tabora
  • Utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana na sisi

    Halmashauri ya Wilaya ya Nzega (Kata ya Utwigu kijiji cha Mwambaha Lubisu )

    Anuani ya Posta: S.L.P 4

    Telephone: 026 2692349

    Simu ya Kiganjani: 0765600994

    Barua pepe: md@nzegadc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hati miliki Halmashauri ya Wilaya ya Nzega @ 2017. Haki zote zimehifadhiwa